Team Job ambayo iko chini ya beki Dickson Job wa Yanga imeibuka na ushindi wa penati 4-2 dhidi ya Team Kibwana iliyo chini ya Kibwana Shomary baada ya sare ya 2-2 katika muda wa kawaida, ukiwa ni mchezo wa hisani kusaidia afya ya uzazi ikienda kwa jina la #WapeTabasamu .

Yamefungwa magoli manne na wachezjazi wawili katika muda wa kawaida…. Wachezaji hao ni Abdul Suleiman Sopu akiifungia Team Kibwana magoli mawili dakika ya 23 na 50 huku Saimon Msuva akichomoa magoli yote mawili dakika ya 74 na 80.

Mechi imepigwa kwenye Dimba la Jamhuri, Morogoro. Tazama highlights…

16 Comments

  1. Haya Mambo yote Ni mazur kwa ajili ya amani ya nchi yetu, Ila nafikiri mtasikia tu hivi punde mikataba mingine ya nchi inafanyika Kama bandari na mingine Kwan wanatuzubaisha na michezo huku wakifanya yao kimiya kimiya

Write A Comment